lirik.web.id
a b c d e f g h i j k l m n o p q r s t u v w x y z 0 1 2 3 4 5 6 7 8 9 #

lirik lagu dizasta vina – uwaridi jeusi

Loading...

williams shakespeare said, speak low if you speak love
no i speak loud because love is war, and war is really loud
i’ll tell you why, the course of true love never did run smooth
love is rough some cupid k!lls with arrows
and some with traps and the point is
you die at the end of the day

yeah nilishare chozi alipolia
baridi ilipomfikia sikukimbia nilishare koti
aliponiletea pozi, niikamzoe nikamkosea
akanuna msamaha nikamwombea airpot

wafanyavyo wazungu nikaonekana mpuzi mkuu
dhahama mbele hadhara uzushi tu
upendo wa dhati ilikuwa script ilikuwa ni uchi
‘cause vyote ilikuwa ni movie tu

nikajajua wamebaki kwenye simulizi
wale wakubaki njia kuu
najua nilisema hivi nao wakanijia juu
tofauti ya hayo maigizo na uhalisia huu
kupendwa kwa hali na mali ni kwenye tamthilia tu

tulioana na picha ikaenda slow slow
aliniambia ananipenda kweli ndivyo
alivyomwambia fredy
kisha akamwambia francy
nami nikamwambia betty fetty
na nancy tukaenda draw draw

hakuna aliyejiforce alie
kati yetu hakuna aliyemdosheaaw machozi mwenzie
hakuwa yeye aliyeziwinda pochi za mashemu
au mimi mwenye namba nyomi za mademu

tukajua kuwa mahusiano sio kitu simple
alliniumiza nikamuumiza tukaishi hivyo
mwanzoni tulichorana mpaka matching tatoos
leo wote ni washenzi nafuu hatukuitikia wito

chorus
nikik~mbuka huwa nataka kulia
watoto na wakubwa wanaaga dunia
kwa sababu wanaumia mama wanaumia
wanaumia mapenzi mabaya
matajiri walisaza dunia
hata masikini wanaotanga na njia
wako ndani wanaumia mama wanaumia
wanaumia mapenzi mabaya

ukweli hakuwaa mbali kuujua
kati yetu hakuna aliyekuwa tayari kukua
niliokota vidonge vya kutoa mimba nikauchubua
akakuta condom kwneye nguo zangu kila alipofua
tukaacha kufanya kwa siri kufanya salama
kila akitaka aishike hatamu
alilala na rafiki yangu rashidi bosi w~ngu kazini
nikalala na dada yeke wa damu

mapenzi noma nakuhusia
shangazi wajomba wanajutia niulize mimi
mapenzi kidonda utaumia
yalimtesa kocha wa dunia mwijuma muumini

hii game ikikushinda buni yako
wanandoa wanafunga ndoa
hawafungi mlango
wakimaanisha kuwa yeyote anaingia
nak~mbuka hata nikimshika
nikimbusu kwa hisia hafumbi macho

mapenzi karaha nyie msije hata kusikia
nishaona wajanja wan~z~acha career
ninapoona wanafunzi nao wanataka ‘dandia
haki ya mama huwa nataka kulia
huwa nataka kulia

nishaona na mke w~ngu ana pete kidoleni
akiwa na mshefa pembenj anasaini lodge anatimba ndani
anaingia mi’ natoka mwili hoi nikiwa nimechoka
pembeni nikiwa na mrembo ananiita honey
akivua pete kwenye milango ya bar
sikuchukia mi mwenyewe nina mipango kando kadhaa
ngoja niwaambie wale wa true love msitaanie
k~mpenda binadamu ni ushujaa nyie

kila alichofanya dhidi yangu
nililipa twende sawa mchongo ndo huo
alichukuwa mababa
mpaka wenye umri wa dingi yangu kuniumiza
nikachukua vitoto vya chuo

aliingilia kushoto niliingilia kulia
alipobuni uongo nami uongo niliujulia
alirudi nyumbani na tai za wanaume tilatila
nikarudi nikiwa na love bite bila bila

na umalaya w~ngu na koti la mtumba
bendi nikakodi na maua rozi ya size kubwa
nikampeleka mke wa mtu lodge
nikazuga ka’ sijaoa na mishumaa
ilibaki kidogo nichome nyumba

hizi romance ni filamu tu
mara nikikuona nasinzia sijui napata homa ya dunia
ni filamu tu
kutembea slow motion hatuwezi
ukimkiss kwenye mvua mvua hainyeshi ni filamu tu
ni filamu tu
kutembea slow motion bado hatuwezi
ukimkiss kwenye mvua mvua hainyeshi ni filamu tu

alishindwa kuuchukua moyo w~ngu auwekeze
nilishindwa k~mfanya awe wife anipendeze
ujanja umeisha uhalisia umeturudisha ndani
tumeathirika na hatujui ndani kauleta nani

ushauri kwa kina dada mahusiano ni vita
wanaume wasafi wapo kwenye vitabu vya kuandikwa
ukiolewa na ndoa ikayumba jiongeze
mwanaume ni mchafu ukitaka aliyetukuka mtengeneze

ushauri kwa kaka mahusiano si hija
wanawake wasafi wapo kwenye filamu za kuigiza
kwahiyo ndoa yako inapopinda jiongeze
mwanamke shetani ukitaka malaika mtengeneze

nikik~mbuka huwa nataka kulia
watoto na wakubwa wanaaga dunia
kwa sababu wanaumia mama wanaumia
wanaumia mapenzi mabaya

matajiri walisaza dunia
hata masikini wanaotanga na njia
wapo ndani wanaumia mama wanaumia
wanaumia mapenzi mabaya
wanaumia mama wanaumia
wanaumia mapenzi mabaya
wanaumia mama wanaumia
wanaumia mapenzi mabaya


Lirik lagu lainnya:

LIRIK YANG LAGI HITS MINGGU INI

Loading...