lirik.web.id
a b c d e f g h i j k l m n o p q r s t u v w x y z 0 1 2 3 4 5 6 7 8 9 #

lirik lagu dizasta vina – tomorrow

Loading...

tomorrow lyrics
verse 1
kesho nafasi ya kuanza upya
k~maliza kuishi nafasi ya kuanza kufa
kuivunja sheria nafasi ya kufuata ruksa
kuik~mbuka jana au kuanza kuifuata future

future ni leo siku ambayo miti hukimbia
jua hushuka upendo, marafiki hufifia, (hufifia)
wimbi la wanafiki huingia
kesho ya tumaini hubakia

tumaini, shika walau shika walau
na ujifunze kuziba kombe pindi anapopita nyang’au
akishapita tenda wema halafu kisha sahau
na uchunge unaponena watakuzika wadau

wadau, walikua uchi ukawavika mavazi
nyumba yako ikavunjika wakakunyima hifadhi
je, utasamehe utasahau kulipa kisasi
au kesho itakukuta umeshika risasi

risasi inawaza wapi itakukutia kesho
utatoroka kambi ama utavungia ghetto
tusipofikia lengo, utahama ukoo kwa kitu kidogo au utaitumikia nembo

nembo ya mjeshi ninayekaza mwendo kishujaa
kama unavyokaza nyonga kwenye tendo la zinaa
napiga goti nashukuru uwepo wa sanaa
kihisia nawapeleka kesho majamaa
majamaa walikua wavivu hawakukazana
waliishia kuamini kuwa kuna wingu la laana
waliseti mipango ila siku hazikufanana
huwezi kuikabili kesho kwa mbinu za jana

chorus
wanasema tomorrow is the mistry
wanasema tomorrow
leo zawadi k~mbatia jana ni history
ya jana hayawеzi yakafana kwenye script hii
wanasema tomorrow is thе mistry
wanasema tomorrow
leo zawadi k~mbatia jana ni history
ya jana hayawezi yaka…

verse 2
nakuletea logic penye faith
nitakutazama ukisha hama
nakuletea topic kai~debet
ninakunyima msosi kwenye plate
njaa ya kesho ikufunze kuheshimu pochi yenye pay

pay huna unatia neno kwenye bao
ukirudi unalalama kuhusu kesho ya wanao
myahudi ukisujudu kwenye uwepo wa farao
kwa wayahudi utaishia kwenye tempo ya karao
karao kazikwa kama historia ulivyozikwa na jana
kesho ni siku ya kujitwika lawama
kesho ni mbali natumai nitafika salama
najipa moyo kisha ninaibusu picha ya mama

mama sishiki simu wakati na~drive
sitii vocha na mafuta full tank kwa gari
sisikii woga, big g za kutosha
chupa za maji na diclopa
na cd za mziki wa papii kocha

kocha kasema kesho nataka bidii tosha
nawaeleza watu w~ngu na bado hawasikii hoja
wamesahau kesho ni nini
niliwaamini leo najuta, ila kesho sirudii kosa

kosa ni kuchoka maana akili haifikiri
taswira kesho naiona na mboni hazihimili
kelele zimeshamili masikio yameshaota
na mdomo unaropoka, dunia haina siri

siri ikasambaa, viganja vikanakili
miguu ikalemaa, ila ubongo ulikalili
tumbo halikujaa na mwili haukunawili
kesho ifike mapema inikute nipo kamili


Lirik lagu lainnya:

LIRIK YANG LAGI HITS MINGGU INI

Loading...