lirik.web.id
a b c d e f g h i j k l m n o p q r s t u v w x y z 0 1 2 3 4 5 6 7 8 9 #

lirik lagu dizasta vina – kibabu na binti

Loading...

mhoji: “mmhh… kwahiyo ni nini kilikujia akilini aah!! mara ya kwanza ulipomuona kibabu?”

binti: “mh….pesa, eeh! pesa. suti aliyovaa, gari anayoendesha, vyote viliongesha kuwa ana pesa”

mhoji: “aah okay..!! sasa ina maana hukujali vitu vingine?”

binti: “ mhh! hapana. umri, background yake, kazi yake, havinihusu. as long as ana pesa”

msimuliaji:

ah
binti akaweka pozi matata
kibabu akaona huu ni msosi akaja
binti akamkonyeza kibabu, kibabu akajibu
kibabu akafungua pochi binti akiifungua zipu

binti akavua nguo zake za mwili akideka
akimwacha yule kibabu tajiri akitweta
hakujali kuitwa malaya hakuona haya
kwa maana akili yake iliwaza pesa

akathibitisha kibabu ana sumni za kutupa
alikuwa na mvi kuonyesha umri pia ni mkubwa
akajisemea “kibabu anafaa kuwa baba yangu
ni ajabu kuona anapiga tour kwa machangu”
akaendelea kuwaza “labda pengine hana mke
kwamba ndo’ maana huu utamu anaufata nje?
au mkewe ni mvivu utamu anaupata nusu?”
akaacha kuwaza baada ya kugundua hayamuhusu

binti akalikabidhi tunda
ilikuwa shughuli kamili shahidi kuta
alijituma kuigiza furaha ilipobidi
aishinde dhiki maana babu alimuahidi bunda

binti akaweka mashauzi ki~star mpaka
kibabu akaenda round kadhaa hata
vyumba vya jirani wote walishtuka
k~msikiliza babu anatoa sauti za raha ah!

na sisi mashahidi tulikuwepo
na hii ndio inafanya hii hadithi iwe special
binti aliwaza leo, hakuik~mbuka jana na upeo wake
hauk~mruhusu kuitabiri kesho

mhoji: “aah okay kibabu”

kibabu: “mh ndiyo”

mhoji: “kwanza naruhusiwa kukuita kibabu? maana najua hilo sio jina lako halisi”
kibabu: “ heh! he heee! aah hapana shida, hapana shida nimekuwa nikiitwa hilo jina kwa muda mrefu na vijana wananitania…kwahiyo hakuna shida unaweza tu ukaniita kibabu”

mhoji: “mh okay basi nitakuita kibabu na nilitaka kujua ni kawaida yako kuwa unanunua hawa madada wanaojiuza au ni mpenzi wa kutembelea haya maeneo mara kwa mara?”

kibabu: “mmmh! kwakweli siwezi kusema ni tabia yangu, mhh hapana, j~po nimefanya mara mbili mara tatu. siwezi kusema nafanya ninafanya hivyo mara kwa mara kwamba ni tabia yangu lakini ni….ukishaoa utajua kwamba kuna muda ndoa ina changamoto za hapa na pale…alafu uta.. unafahamu wewe ni mwanaume”

msimuliaji:

ah! kibabu akaliona pozi matata
kwakuwa ana noti hakuona ugomvi k~mfata
kibabu akakonyezwa kibabu akaji
akaifungua pochi kuona binti akiifungua zipu

kibabu alitokwa na mate
hata noti zilizomtoka si chache
hakufikiri ada za watoto za masomo
alisahau yote kwa maana ubongo uliwaza ngono

akamtazama yule binti maridadi
akajiuliza “vipi kaichagua hii kazi”
na umri wake ni mdogo anaweza kuwa binti yangu
ni ajabu kuona ngono anashiriki na vibabu” ah

“ah au labda ameondokewa na wazazi!
au wapo ila amelelewa kijambazi
au hali ngumu au usawa hauruhusu?”
akaacha kuwaza baada ya kugundua hayamuhusu
kibabu akaonyeshwa njia ya mwezini
akampamba binti pesa ka’ malkia enzini
alikuwa ka’ karogwa raha zilimzonga bila
uwoga akajitosa kuingia penzini

ah na sisi tuliosimuliwa tuliokuwepo
ndio inayofanya hii hadithi iwe special
babu aliwaza leo hakuik~mbuka jana na
umri wake ulifanya asitake kuiwaza kesho
ah!

mhoji: “mh!!! mhu! okay!? okay!! okay!! mmh mnaniacha njiapanda!! eeh…
na hivi ni lini hasa mlikuja kugundua kuwa ninyi ni mtu na binti yake!??”

binti: ……
kibabu: ……


Lirik lagu lainnya:

LIRIK YANG LAGI HITS MINGGU INI

Loading...