lirik.web.id
a b c d e f g h i j k l m n o p q r s t u v w x y z 0 1 2 3 4 5 6 7 8 9 #

lirik lagu dizasta vina – hatia

Loading...

ah.!
niambie ilianza vipi najua haikuanza ghafla
zipi dalili maana hata mafua huanza na chafya
kivipi mi kaka’ako na ulisita kuniambia ukafanya siri ina maana kimsingi nawe ulitaka

ah! kimsingi nawe ulitaka k-mbuka
tangu baba mzee muggo anakufa
alituusia uaminifu na ndio nguzo uliyoiangusha
nashangaa bado nafsi yako hijasuta

maana bado natamani kukujali
mdogo w-ngu natamani sana lakini imani yangu imekufa tayari
sometimes nakwenda mbali
natamani kukudhuru busara inaniweka huru nagundua mi sio mshari

ulianza vipi k-mtamani wife je ni siku namwoa?
au ulianza kabla ya siku ya ndoa
na ndio maana siku ya harusi ushirikiano ilikuwa ni ishu kutoa
kama harusi ni pingu nang’oa

sihitaji tena
najiuliza kwanini nilibashiri
lakini nikapuuzia dalili
kwanini nili….. ah
it all makes sense now

subiri mwanaizaya subiri it all makes sense now
mwezi wa pili hanipi penzi now
yaani kipindi nashusha pensi down
ananiambia kuwa amechoka anahisi kama homa hawezi… how??

(nimiminie wisky)
sikujua kuwaacha pamoja home ilikuwa ni risky
that’s why i’ve been away for so long and she never missed me

sikiza…
sijui unachofikiri rohoni bado
maana upo kimya niseme huoni mwisho huoni mwanzo
ulikataa kusoma chuoni ng’ambo
ubaki ule ninapokula kweli kikulacho ki nguoni mwako

tulisimama kama mdogo na kaka umeng’oa nguzo
hongera kwakuwa mpumbavu yanipasa kutoa tuzo
have you started using cannabis??
man i thought we are brothers
i thought we are bond now we are enemies
enemies…

hii maradufu imeniumiza
acha uliponiangushia mninga
au ulipogusa mzinga nikakuokoa
upole ulizidi ukaniona mjinga
ukaamua k-mshika sharubu simba

ah! remember we use to build a snowman
go school together playing ball and
i can’t believe that my own brother sheg my own wife on my own bed
( on my own bed..)

nilitaka tuwe saresare
ningaefadhiri mbuzi ningekuacha uwe palepale
mabinti hawaishi ukianza huwamalizi ukasahau visima vingi ila maji ni yaleyale

tulikuwa kama mwiko na wali
ulikuwa kijana mzuri mdogo nakuvusha kijito cha maji
umebadilika umepoteza nguvu na ufanisi
mtaa mzima unatembeza rungu kama mlinzi

nilijitoa sadaka ili ufike far
maana sikutaka ikufike njaa
hukutaka unisikilize na
ukachagua kuvunja moyo w-ngu vipande i don’t even know where the other pieces are

vile niliamua kukulea
ah nikakulea kama yai kama…
ukaamua kunionea

kaa kimya.. kaa kimya ngoja nibonge
we ni mdogo w-ngu toka nitoke
inaniumiza sikukwambia tangu mwanzo kwamba huu mwaka wa tatu mi na wife…
tunagonga vidonge

oh men she k!lled you
that devil k!lled you
labda nimeekuua mwenyewe labda ningekuambia kuwa.. kuwa sisi ni waathirika ila nikasita….
men i’m still a fool

yes i’m still a fool..

nikiandika overall summary
nimekuwa mjinga ’cause i k!lled my own family

(nimekuwa mjinga ’cause i k!lled my own family…)

kwakuwa nimekulea nimewajibika
umesoma umepata kazi ya kuheshimika
nahisi kama kazi yangu imekwisha nimemaliza, naondoka naenda mbali maana kuwaona inaniumiza

zingatieni tiba…

(zingatieni tiba…)

(zingatieni tiba….)

k-mbuka kuugua sio kufa.. niahidi hautajuta..

kwaheri


Lirik lagu lainnya:

LIRIK YANG LAGI HITS MINGGU INI

Loading...