
lirik lagu rapcha - dhahabu
[intro: damian soul & rapcha]
takataka
takata
takataka
takata
takataka (what is dead may never die.. what is dead may ne..?)
imetakata
takataka
imekua dhahabu yang’aa
[verse 1: rapcha]
mshua kutumia tu kondomu yeye alikataa
alivyopewa story kuna mimba yangu alikataa
ikabidi mama ndo anipambae j~po mwanzo alipoulizwa home ka’ anamimba ‘ye alikataa
siku zikamove mara miezi ikajikataa
shule walipojua kuwa ana mimba tu wakamkataa
mwisho wa siku mama ndo akajifungua
maana hakupokea ushauri wa kutoa mimba ye alikataa
ado ado kabla ya kutembea nikaanza kutambaa
mama hakutoa macho yake kw~ngu kila saa
akipata dili za chapaa aliomba ndugu zake waangalie mtoto ye atoke wote wakakataa
kwa sababu zisizonihusu, majirani kuruhusu ncheze na watoto wao tu walikataa
mvua zikanyesha zikakata nikakua
nikagundua kuwa mshua hakuzingua
[chorus]
ona takataka leo imetakata
takataka sasa imetakata
takataka
imetakata
takataka
imekua dhahabu yang’aa
[verse 2]
nikaenda shule mwalimu wa hesabu akanikataa
group discussion wale smart wananikataa
nkaanza kujifunza kutongoza sio shule wala mtaa kila binti nnaemtaka ananikataa
kuna ambao kuongea na mimi tu wakakataa
wеngine wakaongea ila kunipa namba wakakataa
wenginе walinipa kwenye kukutana wakakataa
wengine ndo baada ya kuonana wakanikataa
nkitafuta nafasi ya kushine watu wananikataa
nkiwa lowkey ninaboa wananikataa
vyeti nimetembeza ka’ kahawa maofisini
mpaka nguo zangu wamekariri bado wamenikataa
watu wananiambia kuwa kujiriajiri ndo inafaa
nikijiajiri naona kama watu wananikataa
jua linaibuka linazama juu natazama
haya maisha mungu tu pekee ndo hajanikataa
[chorus]
ona takataka leo imetakata
takataka sasa imetakata
takataka
imetakata
takataka
imekua dhahabu yang’aa
[verse 3]
kama hukuelewa ule mstari wa mwisho kwenye verse ya kwanza skia
acha niiweke very clear
mshua alizingua tu kwa kile alichofanya pale ambapo ile story ya mimba yangu ilimfikia
mama nae naona hakuwa proud kunibeba muda ule na ndo maana kwa wazazi alikana akaninificha
all my life all my life all my life
nitatoka jasho nipende sipendi all my life
posa hazina idadi nimetuma karibia niimalize dar
leo wazazi watakubali binti atakataa
ntapoenda kesho binti atakubali wazazi watakataa
kama wote watakubali dini zinakataa
nimeamua kujipenda mimi kwanza
kwa kufanya hivyo siumizwi na yeyote anaenikataa
dunia in~z~di kuzunguka natusua
nagundua nahitaji kusamehe walionikataa
[chorus]
ona takataka leo imetakata
takataka sasa imetakata
takataka
imetakata
takataka
imekua dhahabu yang’aa
[outro: damian soul & rapcha]
takata
takata
(what is dead may never die.. what is dead may ne..??)
imetakata
takataka imetakata
takataka
imekua dhahabu yang’aa
Lirik lagu lainnya:
- lirik lagu zeekayo - серые дома (grey houses)
- lirik lagu radiolucent - all i want
- lirik lagu bryan montero - hola bebe
- lirik lagu wealthy (rapper) - fucked up
- lirik lagu ethn reis - don't stop
- lirik lagu key glock - the grinch
- lirik lagu скажи щось погане (say momething bad) - петля (loop)
- lirik lagu beastboi. - weapon x
- lirik lagu channeldrive - trying
- lirik lagu ivo linna - rublane ring