
lirik lagu dizasta vina - theluji
anachota kwa vidole viwili
anachemsha kwa kijiko inanawili
inakuwa nyevu, anachukua bomba la sindano anaivuta
inajaa kisha anadunga mwili
akili inahama anaita stimu
radha tofauti, sawa na sukari na ndimu
kila stimu ikiisha anajiongezea
anazoea mwili unanasa anaanza kubobea
anajaribu kuacha anairudia
mwili unamlilia uraibu unamvizia
hataki uhalisia maana haujamvutia
anajianzishia uhalisi bandia
anasema
mwili unapoa akili inatosha tufani
kihali gani chombo akidondoka rubani
alitaka furaha, furaha imegota tutani
dawa inampa amani, amani aliyokosa nyumbani
anapoteza sura ya kisomo
anapoteza kazi, hamu ya chakula na ngono
raha anayoipata inakuwa siri yake
kiasi anauza mali kukidhi haja za mwili wake
muuzaji anaendelea kuuza
serikali inaendelea kuzuga
jamii inaendelea kuvunga
washikaji wanaendelea kuvuta
mtaa unaendelea kufa
usimuuzie madawa mwanangu
najua hii kazi inakupa mafao
tafakari yatamkuta mwanao
usimuuzie madawa mwanangu
starehe yake mpya inamvunja pochi
inamaliza afya lakini inamfuta chozi
inamweka mahala pasipoguswa na mwokozi
bahati mbaya damu inawasha anakuna ngozi
theluji inamfikisha mbinguni vyema
anaihusudu hali
kiasi anashuka anaiba mpaka mali ili arudi tena
anaisujudu ganzi
alikuwa na mchumba
walishare all the nice things you know?
dinner dates ice creams
walienda kwenye bata za mjini, k~mbi za movie
kuangalia sijui the black panthers sijui the vikings
leo yupo ila hatamaniki
haangaliki
bora angekuwa malaya au mlevi wa bapa nyingi
ningeelewa, leo ngada zinamfanya anakata ringi
wanasiasa wanabishana
mchungaji ibadani na polisi ofisini
wafanyabiashara wana idhini
na mtaani madawa
yanaendelea kuwalaza chini vijana
najua biashara inakupa mafao
kiasi kwamba unawaza jinsi kutupa mbachao
lakini usimuuzie ngada mwanangu
labda kesho yatamkuta mwanao, just think about it
labda hauna elimu sana
naomba tuongee ka’ wazazi maana
nimeuchoka huu ubazazi
unaofanya nahisi umepitwa na wakati
na unajua nakuheshimu mwana
sina nguvu ningekupeleka mahakamani, ila
uchumi wetu haufanani
mpambanaji leo nashindwa vitani
namzika mwanangu ‘asa mi’ nitazikwa na nani?
swali, una nguvu? ndio
haufanyi chochote kutafuta suluhu? sio
hauko mahabusu, familia yako tukufu
kwa hiyo unahisi haya mambo hayakuhusu, au sio?
usimuuzie madawa mwanangu
labda hii kazi inakupa mafao
tafakari yatamkuta mwanao
just think about it
Lirik lagu lainnya:
- lirik lagu kubilay karça - susmayı öğrendim
- lirik lagu yves - ex machina (english version)
- lirik lagu xhylo - ghost
- lirik lagu silas short - lushland
- lirik lagu lovixx - neon
- lirik lagu marixa balli - pídeme tres deseos
- lirik lagu slump audios & stiffy - si yo le doy bien
- lirik lagu blessd - tti (tú te imaginas)
- lirik lagu puppy angst - in sensitivity
- lirik lagu vegedream - baby mama